Friday, January 14, 2011

MAKAMANDA ARUSHA LEMA NA MBOWE

Mwenyekiti wa CHADEMA na Mbunge wa Jimbo la Hai, Freeman Aikaeli Mbowe.
Habari zilizotufikia hivi punde zinasema kuwa Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendelea (CHADEMA) ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Hai, Freeman Aikaeli Mbowe na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema wametiwa mikononi mwa polisi baada ya kufanya maandamano yaliyozuiwa na Jeshi la Polisi mkoani Arusha.
Chanzo cha maandamano hayo yaliyozaa yote hayo ni kufuatia kitendo cha chama hicho kupinga matokeo ya nafasi ya umeya ya Arusha Mjini ambayo hawakubaliani nayo.
Godbless Lema Mbunge wa Arusha Mjini.

No comments:

Post a Comment