Monday, October 18, 2010

TANZANIA HATARINI KUVAMIWA NA MAREKANI

HALI NI TETE
IOKOE NCHI YAKO KUTOKA KWENYE UTAWALA BANDIA

Habari za uhakika tulizozipata masaa machache yaliyopita ni kwamba JK ameingia mkataba na nchi moja kubwa ili shirika la ujasusi la nchi hiyo liweze kumsaidia kupata ushindi kwa wizi bila kuhatarisha amani nchini. Hii ni baada ya balozi wa nchi hiyo kubwa kumpa ripoti ya kijasusi inayoonyesha kuwa bila usaidizi wa nchi hiyo nchi ni lazima itaingia kwenye vita ndani ya Mwezi Novemba.

Katika ripoti ya shirika hilo la kijasusi imeonyesha kwamba Taasisi ya kijasusi ya Tanzania ama 'idara ya usalama' ukiondoa mkuu wake OR hawana mapenzi kabisa na JK japo kuna wenye mapenzi na CCM. Ripoti hiyo pia imeonyesha kuwa ndani ya vyombo vya usalama na ulinzi ikiwemo JWTZ wana chuki kubwa na JK na wanamdharau kutokana na namna alivyoendesha nchi kwa miaka 5 iliyopita.

Ripoti pia inaonyesha kuwa wanamtandao wa 2005 tayari wanaendesha kwa siri kubwa mchakato wa kijasusi utakaomfanya JK apate 'suprise' kwa kujikuta ameshindwa kabisa kiti cha urais japo mikakati yote ya kuchakachua matokeo imeonekana kufanikiwa. Hili ni kundi lililokuwa nyuma ya uanzishwaji wa CCJ kwa usiri na kwa kujificha.

Ripoti imemtaja EL ambaye majuzi alisifiwa na JK na kutambulishwa kwa wapiga kura huko kaskazini mwa Tanzania kuwa ni mmoja kati ya viongozi wa mkakati huu na ambaye tayari amejiandaa kuhakikisha hata jimboni kwake tu ni yeye peke yake anayepita kwa kushinda kiti cha ubunge lakini JK katu hapiti.

Yako mambo mengi kwenye ripoti hiyo ambayo yalimfanya JK ashindwe kutoa jibu mara baada ya kukabidhiwa ripoti ya mwisho ya REDET na mwanamke mmoja BK wa REDET ambapo hii ilikuwa mara ya pili, kwani mara ya kwanza ilionyesha kuwa JK anaongoza kwa asilimia 81.3 na ndipo baada ya kuangalia upepo akawarudishia ili wairekebishe kwani Dk.alionekana kupata asilimia 6.8 tu jambo lililomfanya JK ang'ake 'wewe unataka kuniharibia wewe, ukimpa asilimia sita si itaonekana uongo wa wazi, kabadilisheni haraka'

Safari hii ilipoletwa alikuwa tayari ameshachanganywa na ripoti ya shirika lile la ujasusi na hivyo baada ya kumgandisha kwa muda mrefu mama huyo ambaye inasemekana ni girlfriend wake wa muda mrefu na ameshaahidiwa ukatibu mkuu wa wizara ya elimu, JK alimwambia tu 'haya kaitoeni' bila kuiangalia kiundani.

Habari zinasema kuwa nchi hiyo kubwa ina uchu mkubwa wa madini yetu ya Uranium na haiko tayari kuona nchi nyingine yeyote inayakamata. Hivyo tayari wamekwisha sambaza NGO zao sehemu kubwa ya Tanzania wakijifanya kushughulikia HIV, kumbe wanafanya ujasusi kuhusu rasilimali zetu. Hawa ni magaidi ambao hupenda kuita nchi nyingine magaidi huku wakiwaibia rasilimali zao.

Hivi sasa wameleta na wanaendelea kuleta majasusi wa shirika lao japo wana utaifa wa nchi mbalimbali kama waangalizi wa kimataifa wa uchaguzi huu ikiwa ni moja kati ya mkakati wa shirika hilo la ujasusi kuhakikisha linatimiza makubaliano ya mkataba, yaani kazi imeanza. Hivyo hata uchaguzi uchakachuliwe mpaka mtoto mchanga mwenyewe aone waziwazi kuwa umechakachuliwa bado waangalizi hao watasema ulikuwa huru na wa haki.

Hivi sasa shughuli za saidia JK ashinde zimeanza pole pole kuchukuliwa na shirika hilo kutoka kwa mtandao mpya wa JK unaoongozwa na RK, na shughuli za kampeni zinazoongozwa na AK. 'we are taking over from here gentlemen' wanasema majasusi hao.

Katika mitambo yetu tumenasa mazungumzo ya ndani ya shirika hilo la ujasusi na inavyoonekana lengo kubwa siyo Uranium peke yake bali ni kufanya undumilakuwili(double crossing) kwa kusaidia JK halafu mlango wa nyuma maadui zake ili kuliingiza taifa hili kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe. Inasemekana kuwa nchi hiyo imefanya ujasusi wa kutosha wa kiuchumi na kugundua kuwa nchi yao itafaidika sana kama Tanzania ikiwa vitani kuliko hali ikiwa ya amani. Wanahitaji Uranium lakini baadaye wanataka waipate kwa njia za panya, halafu wauze silaha na mengineyo.

Nchi hii kubwa inaamini kuwa hakuna biashara inayolipa duniani kama vita. Lakini hawakubali asilani vita kwenye ardhi yao.

Mtaji wao mkubwa kutokana na habari za uhakika kutokwa kwa mmoja wa makatibu wa kwanza wa ubalozi huo ni kwa uchakachuaji wa matokeo.

WATANZANIA TUAMKE, JWTZ, TISS NA WENGINEO KUMBE SIYO WALINZI KWENYE UCHAGUZI HUU BALI NDIO WATAKAO TUMIWA NA NCHI HII KUBWA KULETA MACHAFUKO NCHINI. HAITAKUWA VITA KATI YA WANANCHI NA WANANCHI, ITAKUWA VITA KATI YA JWTZ A NA JWTZ B LAKINI WATAKAOUMIA NI WANANCHI WA TANZANIA KWA FAIDA YA WAGENI.

KAMA UNAIPENDA NCHI HII, ZUIA UCHAKACHUAJI WA MATOKEO AMBAO UMESHAANZA KWA MATOKEO YA TAFITI ZA KISHENZI. VINGINEVYO MUDA SI MREFU........ TANZANIA PIA TUTAITWA NCHI YA KIGAIDI, HUKU JAMAA WAKIBEBA URANIUM, TANZANITE, DHAHABU, ALMASI, WANYAMA WETU, HALAFU HAWATOKI NG'O WAKIDAI KULINDA AMANI MPAKA WAMALIZE KABISA KWA FAIDA YA NCHI ZAO.

JAMANI EBU TUKUBALI MABADILIKO, TUKUBALI SAUTI YA UMMA, VINGINEVYO TUTAJUTA.


IOKOE NCHI YAKO KUTOKA KWENYE UTAWALA BANDIA

TAARIFA HII NI KUTOKA NDANI YA TISS, UPANDE WA WALE WALIOCHOSHWA NA UTAWALA WA JK NA WAFUASI WAKE “CONSERVATIVE HOI POLLOI
My Take:

Nimeipata hii habari kutoka kwa rafiki yangu through email. Sina uhakika na kinachosemwa kama ni kweli, lakini kwetu hapa Bongo kila kitu kinawezekana. Hivi kweli JK anaweza kufikia hatua hii? Tujadili!!! Inasemekana source yake ni TISS kama inavyosomeka hapo juu.

No comments:

Post a Comment